HALI YA NYOTA NEYMAR KUELEKEA KOMBE LA DUNIA BAADA YA VIPIMO



Mshambuliaji nyota wa timu ya Taifa ya Brazil na PSG ya Ufaransa, Neymar Junior, amefanyiwa vipimo vya afya na tayari ameshaungana na wenzake mazoezini kujiandaa na michuano ya Kombe la Dunia huko Urusi.

Neymar alikuwa hayupo fiti tangu aumie katika mchezo wa ligi ya mabingwa Ulaya wakati PSG ilipokutana na Real Madrid kwenye hatua ya 16 bora.

Kuumia kwa Neymar kulizua hofu kama angekuwa na uwezekano wa kuwepo kwenye kikosi cha Brazil kitakachoshiriki michuano ya Kombe la Dunia kwa mwaka huu Russia.

Tayari mchezaji huyo ameshaanza mazoezi baada ya vipimo vya afya kusoma kuwa yupo fiti kwa ajili ya michuano hiyo.

Prepared By DOZEEH BRAND
Share on Google Plus

About Anonymous

0 komentar:

Post a Comment